
Msanii mahiri muziki wenye mahadhi ya Kilingala kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo, JP Mpiana amewasili nchini usiku wa kuamkia leo, ambapo baadaye jioni hii atafanya onyesho kwenye ukumbi wa Ubungo Plaza.
Mpiana aliwasili sambamba na kundi la wasanii wake na kupokelewa na wenyeji wake kampuni ya Sigara, ambapo onyesho lake litafanikishwa kupitia sigara ya Embassy, alisema meneja msaidizi wa bidhaa hiyo, Elizabeth Ndosi.

No comments:
Post a Comment